News

May 8th, 2012
Application Form
April 16th, 2012
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi yasherehekea miaka 50 ya Uhuru
April 12th, 2012
Mhe. Prof. Anna Tibaijuka (Mgeni rasmi ) katika sherehe hizo

Extra Menu

MKUTANO WA RCMRD WAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

Submitted by alexkaraba on Mon, 11/21/2011 - 14:41
Mkutano wa Nchi 18 wananchama wa Upimaji na Ramani wa Raslimali kwa Maendeleo
RCMRD

 MKUTANO WA RCMRD WAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM
Mkutano wa Nchi 18 wananchama wa Upimaji na Ramani wa Raslimali kwa Maendeleo (RCMRD) umefunguliwa jana (17/11/2011) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bw. Patrick Rutabanzibwa jijini  Dar es salaam. Mkutana huo ulihusisha Makatibu Wakuu  wa  wizara zinazohusika na ardhi wa nchi hizo na wataalamu wa upimaji na ramani ikiwa ni baada ya kikao cha maandalizi cha wataalam hao mapema wiki hii.

 

 Pichani  kulia ni Mwenyekiti wa mkutano Dr. S. D. Mqayunga na  kushoto ni Mkurugenzi Mkuu RCMRD Dr, Hussein O Farah(Picha na Anna Massao). Picha iliyoko chini inaonesha baadhi ya Wajumbe wa nchi wakisikiliza meza kuu.
(Picha na Anna Massao)

 Lengo kubwa la mkutano huu ni kusaidia nchi za Afrika katika masuala ya upimaji na ramani kwa ajili ya maendeleo. Mkutano huu ni wa 45 kufanyika baada ya ule wa Capetown, South Afrika. Makao makuu ya RCRMD yako jijini Nairobi na Tanzania ni miongoni mwa waanzilishi wa kituo hiki mwaka 1975. Hadi sasa RCRMD Inajumuisha nchi kumi na nane zikiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, Sudan, Ethiopia, Botswana ,Namibia ,Zambia, Mauritius, Seychelles , Somalia, Comoros , South Africa, Rwanda, Burundi , Lesotho ,Malawi na Swaziland.

Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye pia ni Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani katika  Wizara ya ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Bw. Silas Mayunga anasema, ‘tunafarijika kupata fursa ya kuaandaa mkutano huu, maazimio yatasaidia katika kuimarisha shughuli za upimaji ardhi, utunzaji wa mazingira na mafunzo kwa wataalamu na pia nchi yetu imejitangaza.

Bwana  Mayunga  aliongeza kuwa Tanzania ni nchi ya kwanza barani Afrika  kukamilisha mpango wa alama ya upimaji ardhi inayojulikana kitaalamu ‘geodetic network’ambazo ni 740 na kuweza kusimikwa nchi nzima na kuongeza kuwa 6 kati ya alama hizo zimepimwa kitaalamu kwa njia ya satelaiti na pia serikali ina mpango wa miaka mitano wa upimaji ardhi nchini na katika kutekeleza mpango huo serikali imekubali kuanzisha kituo cha kupokea picha za satelaiti kitakachojengwa mjini Dodoma.